0
NMB yatoa milioni 100 kudhamini mkutano mkuu wa 40 wa ALAT
April 22, 2026
Posted 3 hours ago by
Benki ya NMB imetoa udhamini wa Sh milioni 100 kwa ajili ya kusaidia maandalizi na uendeshaji wa Mkutano Mkuu wa 40 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) utakaofanyika jijini Arusha. Udhamini huo unaongeza nguvu katika maandalizi ya mkutano huo muhimu unaotarajiwa kuwakutanisha wajumbe kutoka mamlaka mbalimbali za serikali za mitaa nchini. Makabidhiano ya mfano wa hundi hiyo yalifanywa na Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Baraka Ladislaus, kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mkutano huo, Juma Hokororo, katika hafla iliyoshuhudiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa ALAT, Thomas Vungwa.
Msaada huo unalenga kuchangia kufanikisha mkutano huo wa uchaguzi [] The post NMB yatoa milioni 100 kudhamini mkutano mkuu wa 40 wa ALAT appeared first on SwahiliTimes.
SwahiliTimes
Coverage and analysis from Tanzania. All insights are generated by our AI narrative analysis engine.